Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
afyatipsMagonjwamagonjwa ya wanaumemagonjwa ya wanawakemagonjwa ya watoto

MADHARA KUPAKA LIPSTICK

MADHARA KUPAKA LIPSTICK

Lipstick 

Na Dr Mathew


Urembo ni kitu kizuri sana na kila mwanadada anapenda aenekane amedamshi na kuvutia ama kwake mwenyewe au marafiki zake na hata wapenzi wao.

Sasa naenda kuelezea kwa ufupi baadhi ya vitu vilivyopo kwenye lipstic na baadhi ya madhara yake.


1) Kiambata Propylparaben:hiki ni mojawapo ya kemikali iliyopo sana kwenye bidhaa hizo. Mojawapo ya madhara yake ni kuunguza na kuchoma choma maeneo ya macho na mdomo,kuharibu mfumo wa mwili wa vichocheo na KANSA.


2) kiambata Methylparaben: Hiki kiambata na maarufu sana na kazi yake kuu ni kutunza(preservative) au kuhifandi lipstic ili ionekane kama ilivyo,mojawapo ya madhara yake ni ngozi kufifia,KANSA nk.


3) kiambata Retinyl Palmitate: Kiambata hiki ni vitamini A ilotengenezwa na hua ipo sana kwenye lipstic,madhara makubwa ya hiki kiambata ni kwa kina mama wajawazito kwani yaweza kusababisha mtoto azaliwe na ulemavu au mimba kutoka.


4) kiambata Tocopheryl Acetate, hii vitamini E ilotengenezwa na kazi yake kubwa ni kuongeza unyevu unyevu uliopo kwenye bidhaa hii.madhara yake ni kuungua,kubabuka,malengelenge,kuwashwa nk


5) kiambata chromium kiambata hiki kinafahamika kama kisababishi kikuu cha kansa ya binadamu na uwezekano wa kupata saratani inafatana na matumizi yake kwa muda mrefu.


6) kiambata Cadmium: inajulikana kama kisababishi kikubwa cha saratani ya mapafu


7) kiambata lead: kila mtu anaelewa lead ni mbaya sana kwa afya zetu.ina madhara kama kuharibu mishipa ya fahamu,mimba kuharibika,matatizo ya kushika mimba,matatizo ya mzunguko wa hedhi nk.


8) Viambata vingine ni phthalates,DMDM hydantoin

BHUT (butylated hydroxytoluene),bronopol,diazoldinyl urea,sodiumhydrozymethylglycinate,imidazolidinyl urea,methenamine,quarternium-15, Quaternium-18, Quaternium-26,butylated compounds (bht, bha),peg compounds,Octinoxate nk ambavo hivi vyote vina madhara makubwa kwa binadamu kama saratani ya dundumio,matatizo ya uzazi,mimba kuharibika,matatizo ya mishipa ya fahamu,kuzaa watoto wenye ulemavu nk.


SASA HAPO NDO MWISHO WA MAELEZO MAFUPI YA MADHARA YA VIAMBATA VILIVYOPO KWENYE LIPSTIC.

EWE MWANAMKE CHUKUA HATUA.

TAG MWANADADA AU MWANAMKE YEYOTE NA UTAKUA UMEMSAIDIA SANA

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!




Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass