Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake,

Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu tatizo hili, na kama una shida hii pia, Mwisho wa Makala hii kuna mawasiliano yote, Tuwasiliane mara moja ili Kupata Msaada.

TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI

Hili ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na tatizo hili huhusisha kuota kwa nyama laini ndani ya kuta za pua na kuzunguka eneo la mwamba wa Pua.

CHANZO CHA KUOTA NYAMA PUANI

Nyama hizi huweza kuota au kutokea ndani ya Pua kwa sababu mbali mbali kama vile;

• Maambukizi  ya magonjwa mbali mbali yanayotokea ndani ya Pua au yanayohusisha mfumo mzima wa hewa

• Tatizo la kusumbuliwa na allergy

• Kutokea kwa Uvimbe ndani ya ngozi laini ya puani au katika mfumo mzima wa hewa

• Kuwa na tatizo La Ugonjwa au shida ya Astha( Pumu)

• Pia kufanya kazi maeneo yanayohusu upuliziaji wa madawa mbali mbali huweza kuchangia uwepo wa tatizo hili

Soma: Tatizo la Kuota kinyama Ukeni-Masundosundo

DALILI ZA KUOTA NYAMA PUANI

– Kuanza kwa Dalili za mafua ya mara kwa mara

– Mgonjwa kushindwa kupumua/kupumua kwa shida au kubanwa kutokana na nyama za puani kuziba nafasi ya hewa kupita Puani.

– Mgonjwa kukoroma

– Mgonjwa kutoa sauti flani wakati wa kuvuta na kutoa Hewa puani

– Wakati mwingine mgonjwa kupata maumivu makali ya meno upande wa juu Pamoja na kuwashwa na Macho

– Mgonjwa kupata tatizo la kushindwa kunusa kitu na kupata harufu ya kitu husika mfano chakula N.k

MATIBABU YA TATIZO HILI LA KUOTA NYAMA PUANI

✓ Tatizo hili la kuota nyama puani huweza kutibika kwa Njia mbili kubwa, Dawa pamoja na Upasuaji.

1. Matibabu ya dawa, huhusisha aina mbali mbali za Dawa kulingana na chanzo cha tatizo hili,

Epuka matumizi ya dawa kabla ya kuongea na Wataalam wa afya kuhusu tatizo lako.

2. Matibabu kwa Njia ya upasuaji huhusisha kuondoa kinyama ambacho kimeziba puani moja kwa moja.

Pamoja na kupewa dawa kwa ajili ya kuzuia maumivu na asipate maambukizi mapya ya magonjwa kwenye kidonda.

Tatizo hili kwa Hivi Sasa linasumbua watu wengi, je wewe umepata Tiba na Kupona kabsa?

Soma: Tatizo la Kuota kinyama Ukeni-Masundosundo

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass