Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
afyatipsMagonjwamagonjwa ya wanaumemagonjwa ya wanawakemagonjwa ya watoto

MTOTO WA JICHO CHANZO CHAKE,DALILI,KINGA NA TIBA YAKE

MTOTO WA JICHO

• • • • • •

Hali ya Mtoto wa Jicho inatokea pale lenzi ya jicho inapopata ukungu na kuathiri uwezo wa kuona. Mtoto wa jicho ndio chanzo kikuu cha upofu kwa watu wenye miaka zaidi ya 40.


CHANZO 

Sababu kubwa ya Mtoto wa Jicho ni umri mkubwa. Kama una umri zaidi ya miaka 40 na unaona hali ya ukungu katika jicho lako basi unaweza kuwa na mtoto wa jicho. Pia mtoto wa jicho inaweza kusababishwa na: ugonjwa wa kisukari, presha ya damu, ajali katika jicho au kukaa muda mrefu kwenye jua kali.


DALILI

Huwa hakuna dalili katika hatua za mwanzo za mtoto wa jicho. Baadaye mtu mwenye mtoto wa jicho huwa anaona ukungu, haoni vizuri nyakati za usiku, pia huwa anasumbuliwa sana na mwanga.


KINGA 

Ulaji mzuri wa mboga, matunda na vyakula vyenye antioxidant unapunguza uwezekano wa kutokea mtoto wa jicho kwa watu wenye umri mkubwa. Pia uvaaji miwani ya jua unasaidia macho kutopatwa na mtoto wa jicho.


TIBA

Hali ya mtoto wa jicho inaweza kutibika kwa kuondoa lenzi yenye ukungu kwa njia ya upasuaji. Ni upasuaji mdogo chini ya dakika 30 ambapo mgojwa anaruhusiwa kurudi nyumbani siku hiyo hiyo.


#afyabongo #drtareeq


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!




Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass