Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Hali ya msanii wa Bongo Muvi, Carina Hussein, imezidi kuwa mbaya tena,afanyiwa upasuaji mara 21

Hali ya msanii wa Bongo Muvi, Carina Hussein, imezidi kuwa mbaya tena, baada ya kufanyiwa upasuaji wa mara ya 21 kutokana na mshono mkubwa wa tumboni kwake kufumuka tena na kinyesi kuanza kutoka mfululizo.

Hali ya msanii huyo imezidi kudhoofika sana tofauti na awali huku akisema kuwa katika operesheni zote alizofanya hii imekuwa ya maumivu sana na kubwa zaidi hajapata haja kubwa karibia mwezi na mkojo hautoki mpaka amewekewa mpira wa kutolea mkojo.

” Nimekuwa kwenye mateso makubwa sana sikuwa napenda tena kueleza maana kama nawachosha watu, lakini ukweli nina maumivu makali na dawa nanunua elfu 92000, kila baada ya siku tatu, bado kubadilisha kidude shingoni zaidi ya laki moja, tumeshauza chochote tulichonacho hatuna hata cha kuuza tena, nateseka jamani” alisema hawa kwa tabu kutokana na kudhoofika sana.

Globaltvonline imefanya naye mahojiano nyumbani kwao Magomeni jijini Dar, na kuona wazi kuwa Carina, anahitaji msaada sana kwa sasa hivyo amewaomba watanzania wasimchoke, anateseka mno amepungua sana, maana hana anachokula kikaa tumboni.

” Nateseka mpaka natamani Mung, afanye chochote juu yangu, sina matumaini tena” alisema Carina

Kama unataka kumsaidia chochote waweza kumsaidia kupitia namba

0769_990045 M-PESA
Carolinhawa Hussein Ebrahim bounin.

0789_095858 Airtel money
FATUMA MIKIDADI maruzuku..

0712_595858 tigopesa
Carolinhawa Hussein Ebrahim bounin

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass