Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Boti yaua watu 94 waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu

Boti yaua watu 94 waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu

Takriban watu 94 wamefariki, 26 hawajulikani waliko nchini Msumbiji baada ya boti isiyokuwa na leseni kupinduka.

Takriban watu 94 wamefariki wakiwemo watoto na wengine 26 hawajulikani walipo baada ya boti ya feri kupinduka katika pwani ya kaskazini mwa Msumbiji.

Boti hiyo ilikuwa imebeba watu waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu unaolikumba taifa hilo la Afrika Mashariki, shirika la utangazaji la serikali TVM liliripoti.

Meli hiyo ilikuwa mashua ya wavuvi iliyojaa kupita kiasi na haikuwa na leseni ya kusafirisha watu, Lourenco Machado, msimamizi wa INSTRASMAR, alisema kwenye Television ya serikali Jumatatu.

“Siku ya Jumapili tulisajili tukio la baharini ambapo takriban watu 94 walikufa wakati mashua iliyokuwa imebeba watu 130 ilipopinduka. Tumepata miili 94 na 26 haipo,” alisema.

Boti hiyo ilikuwa ikisafirisha watu kutoka Lunga katika jimbo la Nampula kwenda Kisiwa cha Msumbiji, alisema, akiongeza kuwa ripoti za awali zilionyesha kuwa ilikumbwa na wimbi kubwa la maji.

Abiria walikuwa wakikimbia mlipuko wa kipindupindu, Lilisema shirika la utangazaji la TVM, likimnukuu msimamizi mwingine wa baharini wa eneo hilo.

Jaime Neto, waziri wa mambo ya nje wa jimbo la Nampula, pia alisema kuwa abiria hao walikuwa wakikimbia kipindupindu.

“Kwa sababu boti hiyo ilikuwa imejaa watu wengi na haikufaa kubeba abiria, iliishia kuzama,” akiongeza kuwa watoto wengi walikuwa miongoni mwa waliofariki.

Credits; TVM

Photos: TVM,LIB, BBC

Editor; @afyaclass

Reviewed by: Dr.Ombeni Mkumbwa

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass