Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

UMUHIMU WA TIKITI MAJI KWA WATU WANAOFANYA MAZOEZI

TIKITI MAJI

• • • • • •

UMUHIMU WA TIKITI MAJI KWA WATU WANAOFANYA MAZOEZI


Watu wengi hawafahamu kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kula tikiti maji,faida za tunda hili ni nyingi katika mwili wa binadamu, ila hapa tunagusia kuhusu umuhimu na faida za tikiti maji kwa mtu ambaye anafanya mazoezi.


Vyovyoye utakavyo kula,either umekula kama tunda lilivyo kwa kutafuna au umetengeneza juici yake bado umuhimu wake mwilini ni ule ule,tofauti ni maandalizi tu  pamoja na matumizi.


– Tunda hili la tikiti maji ni miongoni mwa matunda ambayo yana wingi mkubwa wa maji,hivo husaidia sana kuongeza maji ya mwili na kurudisha kwa kiasi flani kiwango kikubwa cha maji ambacho hupotea kwa njia mbali mbali kama jasho,N.K wakati wa kufanya mazoezi.


– Ndani ya tunda la tikiti maji kuna virutubisho mbali mbali kama vile; Amino acid inayojulikana kwa jina la l-citrulline, ambayo husaidia sana katika kupoozesha misuli yako baada ya kufanya mazoezi. Kumbuka wakati unafanya mazoezi misuli ya mwili hupata moto au joto sana,hivo tunda hili litakusaidia sana.


– Matumizi ya tunda la tikiti Maji au juisi yake kabla hujaanza kufanya mazoezi husaidia sana katika kupunguza maumivu ya misuli ambayo unaweza kuyapata mara tu baada ya kufanya mazoezi, Hivo watu wanaofanya mazoezi mbali mbali kama ya kucheza mpira,kukimbia,N.K huweza kupata faida hizi.

KWA USHAURI ZAIDI AU ELIMU TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.