Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

MADHARA YA MATUMIZI YA ASALI KWA MTOTO MDOGO

MADHARA YA MATUMIZI YA ASALI KWA MTOTO MDOGO
 
Watu wengi hawafahamu kwamba mtoto mdogo hatakiwi kupewa asali kabsa, kuna madhara ambayo huweza kumpata mtoto mdogo kama akiwa anapewa asali mara kwa mara.
 
ATHARI YA ASALI KWA MTOTO MDOGO
 
Kwa watoto ambao wana umri wa chini ya Mwaka Mmoja, huweza kupata madhara wakitumia asali mara kwa mara kutokana na uwepo wa bacteria aina ya Clostridium botulinum kwenye asali.
 
Clostridium botulinum ni bacteria ambao huweza kuwepo ndani ya asali, endapo mtoto mdogo atapewa asali bacteria hawa huweza kupenya moja kwa moja na kuzalisha sumu kali ambayo hufyonzwa katika utumbo wa mtoto na kusababisha tatizo ambalo kitaalam hujulikana kama Infant Botulism.
 
Tatizo hili la Infant botulism huambatana na dalili mbali mbali.
• Dalili ya kwanza kabsa ni mtoto kupata choo kigumu,kupata shida wakati wa kujisaidia au kukosa kabsa choo.
 
•Mwili wa mtoto kukosa nguvu kabsa na kuwa dhaifu
 
• Mtoto kupoteza kabsa hamu ya kunyonya au kula kitu chochote
• Mtoto akilia sauti hutoka kidgo sana au hulia kama mtu ambaye amechoka sana na hana nguvu kabsa
 
• Uwepo wa mtoto kucheza, au movement kwa ujumla hupungua sana
 
• Mtoto kukosa kabsa nguvu ya kunyonya maziwa ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Poor sucking
 
• Ngozi ya mtoto kuanza kuwa  kavu sana na kubadilika rangi
 
• Uwezo wa mtoto kutoa mkojo kupungua kwa kiasi kikubwa au kupatwa na tatizo la urinary retention
 
• Uwezo wa umeng’enyaji wa chakula cha mtoto tumboni kupungua kwa kiasi kikubwa
 
• Mapigo ya moyo kwa mtoto kuanza kubadilika
Hayo ndyo baadhi ya madhara ya matumizi ya asili kwa mtoto mdogo, hivo basi ni wito wangu kwa wazazi au walezi wa watoto kuacha kabsa tabia ya kuwapa watoto wadogo asali kwani ni hatari sana kwa afya zao.
 
Mbali na madhara ambayo nimekwisha yataja hapo juu katika makala hii, Mtoto pia huweza kupoteza maisha kabsa kutokana na madhara ya sumu kali ambayo huzalishwa na bacteria hawa aina ya Clostridium botulinum.
 
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
 
 

 

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.