Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Miongoni mwa vyakula vinavyoweza kukusaidia kwenye kumbukumbu ni hivi vifuatavyo

Miongoni mwa vyakula vinavyoweza kukusaidia kwenye kumbukumbu ni hivi vifuatavyo

1. Zabibu za rangi ya zambarau

Ziko aina kadhaa za zabibu, ambazo maarufu ni zile zenye rangi ya kijani na za rangi ya zambarau. Watafiti wanathibitisha zabibu za zambarau zinamchango mkubwa kwenye kumbukumbu.

Kwa watu wazima wenye matatizo ya kumbukumbu wwakinywa nusu lita ya juice ya zabibu za rangi ya zambarau kila siku kwa muda wa wiki 12 (miezi mitatu) zitawasaidia.

Zabibu za zambarau zina kitu kinaitwa Anthocyanins na Polyphenols vinavyoipa rangi iliyokolezwa ambayo ni muhimu. Polyphenols pia inapatikana kwenye matunda mengine kama Apple na mapeasi.

Wakati wa mmengenyo wa vyakula hivi baada ya kuliwa vinasaidia kuifanya mishipa ya damu kunyumbulika vizuri na kutembea kwa damu kuelekea kwenye ubongo.

2. Blueberries

‘Watoto kula gram 240 (kama robo kilo) ya Blueberries wa kila siku zinawasaidia kukumbuka maneno mengi na kuyakumbuka kwa usahihi masaa mawili baadaye’, anasema Kimberley.

Kima ilivyo kwa zabibu za zambarau Blueberries pia zina kitu Anthocyanins na Polyphenols. Kama inavyofanya zabibu kwenye mishipa ya damu, Blueberries pia inaifanya mishipa ya damu kunyumbulika vizuri na kutembea kwa damu kuelekea kwenye ubongo. Hilo linasaidia kuleta nguvu zaidi, virutubishi na oksijeni.

3. Chocolate

‘Taarifa njema kwa wapenda Chokleti, kwa sababu chokleti zina kakao ambayo inaboresha usambazaji wa damu kwenye akili, lakini inapaswa kuwa ‘dark chocolate’ ambayo ina asilimia 70% ya virutubishi vya kakao (Cocoa solids) ili kupata faida yake’, anasema Kimberley.

Lakini wataalamu wanasema muhimu kula mlo kamili wenye mboga za majani, matunda, protini kama samaki na maharage kwa sababu una faida kubwa kwenye ubongo wa mwanadamu.

4. Grean Tea

Ukiacha kusaidia kukulinda na saratani, hatari ya kupata magonjwa ya moyo, unene pia inasaidia kuboresha afya ya akili.”

Chai hii inafaida kubwa kwenye kumbukumbu. Hasa wenye tatizo la kumbukumbu za muda mfupi, grean tea, inaweza kuwasaidia sana.”

Source:BBC

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.