Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Madhara Mwanamke anaweza kupata kwa Kuvuta SIGARA

Madhara Mwanamke anaweza kupata kwa Kuvuta SIGARA

Madhara ya uvutaji wa sigara ni kwa kila mtu anayevuta bila kujalisha umri au jinsia, japo kuna madhara mengine huwa maalum kwa jinsia flani, Katika makala iliyopita nilielezea madhara ya Sigara kwa wanaume soma hapa..!!

Lakini katika makala ya leo tunazungumzia madhara ya Uvutaji wa sigara Kwa Wanawake.

MADHARA YA MWANAMKE KUVUTA SIGARA NI PAMOJA NA;

1. Uvutaji wa sigara huweza kumuweka mwanamke katika hatari ya kupata shida ya mimba kutunga nje ya kizazi yaani kwa kitaalam tunaita Ectopic pregnancy

2. Uvutaji wa sigara kwa mwanamke huweza kumsababishia kuwa katika hatari ya kupatwa na shida ya kansa mbali mbali

3. Mwanamke kuzaa watoto wenye tatizo la uzito mdogo sana kuliko kawaida(uzito wa kawaida Kgs 2.5 mpaka 3.5)

4. Mwanamke kuwa katika hatari ya kupatwa na tatizo la mvuruguko wa vichocheo vya mwili yaani kwa kitaalam tunaita hormone imbalance

5. Mwanamke kupatwa na shida ya kutokubeba mimba au kushika ujauzito na kutoka wenyewe

6. Kuzaa watoto wenye matatizo katika mfumo mzima wa upumuaji

7. Mwanamke kuzaa watoto wenye shida ya figo

8. Mwanamke kuzaa watoto na kufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa

9. Uvutaji wa sigara huweza kusababisha matatizo ya mapafu ikiwa ni pamoja na Kansa ya mapafu

10. Kupatwa na shida ya koo ikiwa ni pamoja na kupatwa na kansa ya Koo

N.K

ONYO; uvutaji wa Sigara ni hatari kwa afya yako na afya ya mtoto wako

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.