Daktari Mhanga Wa Virusi Vya Marburg Kuzawadiwa Shilingi Milioni 10
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania leo imetangaza kumzawadia kiasi cha shilingi milioni 10 Daktari aliyepata changamoto ya kiafya wakati akiwa kwenye mapambano dhidi ya milipuko wa Ugonjwa wa virusi vya Marburg uliotokea mkoani Kagera Mwezi machi mwaka huu.
Taarifa hiyo imetolewa leo Agosti 7, 2023 mkoani Kagera na Naibu Waziri @wizara_afyatz Mhe.Godwin Moleli wakati wa kikao kazi na wahudumu wa sekta ya Afya katika Mkoa huo
” Nawapongeza wahudumu wetu wa afya kwa kazi kubwa mliyofanya ya kupambana na Ugonjwa huu, hali ilikuwa ya hatari na ngumu lakini mlipambana mno hivyo pokeeni shukrani zetu za dhati”amesema
Ameendelea kufafanua kuwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa huyo kuna Daktari aliyepata changamoto ya kiafya hatuwezi kumuacha hivyo amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa kuanzia kuanza mchakato wa kumpa kiasi cha shilingi milioni kumi ili ziweze kumsaidia katika kipindi hiki kugumu.
“Huyu ni Kama mwanajeshi aliyejeruhuwiwa vitani hivyo hatuwezi kumuacha kabisa”” amesisitiza