Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Wagonjwa 10 Wamefanyiwa Upasuaji Mkubwa wa Moyo wa Kuzibua Mishipa ya Damu iliyoziba

Wagonjwa 10 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa kuzibua mishipa ya damu iliyoziba katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo ya siku saba.

Kambi hiyo iliyomalizika leo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam imefanywa na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa JKCI kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Max iliyopo nchini India.

Akizungumzia kambi hiyo Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema kambi hiyo imefanyika kwa mara ya nne kwa kushirikiana na wataalam kutoka Hospitali ya Max kuwafanyia upasuaji wagonjwa waliohitaji utaalam zaidi kutokana na mioyo yao kuwa na uwezo mdogo wa kufanya kazi.
Dkt. Angela alisema kambi hiyo ililenga kufanya upasuaji mkubwa wa moyo kwa watu wazima ambao wanamishipa ya moyo iliyoziba lakini pia viwango vya ufanyaji kazi wa mioyo yao kuwa chini ya asilimia 30.

“Upasuaji ambao tumewafanyia wagonjwa hawa ni mgumu kidogo, tumekuwa tukiwafanyia uchunguzi wagonjwa hawa na kuwakaribisha wenzetu kutoka Hospitali ya Max ili kwapamoja tuweze kuwahudumia wagonjwa hawa lakini pia tuweze kuongeza ujuzi wetu katika kuwahudumia wagonjwa wa aina hii”,
“Katika kambi hii wagonjwa wamepandikizwa mishipa ya moyo mitatu na wengine zaidi ya mitatu bila ya kuusimamisha moyo kwa mafanikio makubwa hii kwetu sisi ni hatua kubwa katika kutoa huduma kwa wagonjwa wa moyo”, alisema Dkt. Angela

Aidha Dkt. Angela alisema JKCI inategemea kufanya upasuaji wa mshipa mkubwa wa moyo ambao umetanuka, kubadilisha mishipa ya moyo pamoja na kuweka mlango mpya kwa wagonjwa ambao wana matatizo ya mishipa mikubwa ya moyo kutanuka.
Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka Hospitali ya Max iliyopo nchini India Subhash Sinha alisema ushirikiano wake na wataalam wa JKCI unaonyesha mafanikio makubwa tangu walipoanza kushirikiana hadi sasa.

Dkt. Sinha alisema kupitia upasuaji wa moyo ambao amekuwa akifanya na wataalam wa JKCI amekuwa pia akitoa mafunzo na mbinu mbalimbali za kufanya upasuaji mkubwa wa mishipa ya moyo kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yapo chini ya asilimia 30 bila ya kuusimamisha moyo.

Forum Manager

Content creator&editor (Ms.Asifiwe)Jukumu langu kwako ni kuhakikisha unapata elimu ya kutosha pamoja na Updates mbali mbali ndani ya http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.