Maadhimisho ya miaka 77 ya Uhuru nchini India
India kuadhimisha miaka 77 ya Uhuru siku ya Jumanne. Wakati Waziri Mkuu Narendra Modi akitoa hotuba yake ya kila mwaka kutoka Red Fort huko Delhi, watu kote nchini walisherehekea kwa sherehe za bendera na programu za kitamaduni, kuwakumbuka wapigania uhuru wa India.
Mnamo Agosti 14, 1947 – katika mkesha wa uhuru wa India kutoka kwa utawala wa Uingereza – waziri mkuu wa kwanza wa taifa hilo, Jawaharlal Nehru, alipandisha bendera ya taifa kutoka Red Fort huko Delhi ikifuatiwa na hotuba maarufu inayojulikana kama ‘Tryst with Destiny.’
Kampuni ya East India ilichukua udhibiti wa taifa hilo mnamo 1757 baada ya Vita vya Plassey. Karibu karne mbili baadaye, “Harakati ya Kuacha India” ilisababisha Waingereza kuondoka nchini mnamo 1947.
Uhuru ulikuja kwa bei ya mgawanyiko – kwa kuundwa kwa nchi mbili, India na Pakistani – ambayo ilisababisha ghasia na mauaji makubwa na inaendelea kuziandama nchi zote mbili hadi leo.