Makubaliano ya uhusiano kati ya Tanzania na Indonesia
Tanzania imeendelea kunufaika na uhusiano na Indonesia ambapo huuza nchini humo bidhaa za kilimo kama karafuu, pamba, tumbaku, cocoa, karanga, pamoja na madini aina ya shaba, huku Indonesia ikiuza nchini mafuta, vipuri vya mashine, bidhaa za kemikali, karatasi na nguo.
Katika ziara ya siku mbili ya Rais Yoko Widodo wa Indonesia nchini Tanzania moja ya makubaliano ya ushirikiano yatakayosainiwa ni katika biashara, ambapo viongozi wa mataifa yote wamejidhatiti kukuza biashara ili iendane na ukubwa wa historia baina ya mataifa hayo.
Rais Joko Widodo aliwasili nchini jana akitokea Kenya, na pia anatarajiwa kuzuru Msumbiji na Afrika Kusini kama sehemu ya ziara yake ya kwanza barani Afrika.