Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Karim Mandonga kapigwa tena Zanzibar na Bondia Muller Jr

Karim Mandonga kapigwa tena Zanzibar na Bondia Muller Jr:

Bondia Muller Jr ameibuka mshindi kwenye pambano la Raundi Sita dhidi ya Karim Mandonga pambano la Tamasha la Uzinduzi wa Mchezo wa Ngumi Zanzibar lilopigwa katika uwanja wa Mao Tse Tung, Zanzibar.

Muller Jr ameshinda kwa uamuzi wa Majaji na kuwa moja ya walioandika historia ya kushiriki kwenye tukio la kuurejesha tena mchezo wa Masumbwi Zanzibar baada ya miaka 60 kupita bila ya mchezo huo.

Pambano hilo la Raundi Sita limeshuhudiwa na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ambaye alijuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mashindano ya ngumi yaliyopigwa marufuku Kisiwani hapo zaidi ya mika 50 iliyopita ambapo Majaji wote watatu wamempa ushindi Kiluwa kwa pointi 55-56, 56-58 na 55-59

Hii ni mara ya tatu mfululizo Mandonga kupigwa. Julai 22 alipoteza pambano la marudiano na Mkenya Daniel Wanyonyi, na Julai 29 alipoteza pambano dhidi ya mganda Moses Golola na sasa Mandonga anasema anajipanga kwa ajili ya pambano jingine.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.