Wahamiaji 170 Wamerejeshwa Nchini Senegal
Takriban wahamiaji 170 wamerejeshwa nchini Senegal baada ya kuwa njia panda kwa wiki nzima ndani ya boti ya uwokozi ya Uhispania.
Naibu meya wa Dakar Lamine Ndiaye amethibitisha kwamba wahamiaji 168
wamekabidhiwa kwa maafisa wa Senegal.
Tangu Alhamisi wiki iliyopita wahamiaji hao walikuwa wamekwama ndani ya meli ya ulinzi wa raia ya Uhispania karibu na nchi ya Kaskazini Magharibi mwa Afrika ya Mauritania baada ya mamlaka za nchi hiyo kukataa kuwaruhusu kuteremka.
Nini kifanywe kuzuia safari hatari zinazofanywa na wahamiaji wa Kiafrika kujaribu kuingia Ulaya?