TANZIA: Mwimbaji BONGOFLEVA Haitham Kim Amefariki Dunia Ijumaa
TANZIA: Mwimbaji BONGOFLEVA Haitham Kim Amefariki Dunia Ijumaa
Mwimbaji wa Bongofleva Haitham Kim ambaye hivi karibuni Wasanii na Wadau wengine walianzisha kampeni ya kusaidia kuchangisha pesa kwa ajili ya matibabu yake amefariki tarehe 1 Septemba siku ya Ijumaa katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke Jijini Dar es salaam.
BNB ambaye ni Rafiki wa Mume wa Marehemu aliyekuwa akisaidia kumuuguza Haitham, ameithibitishia kuwa ni kweli Haitham amefariki leo Hospitalini hapo.
Bryson ambaye ni Mume wa Marehemu alisema hali ya Haitham ilibadilika ghafla siku saba zilizopita akisumbuliwa na upumuaji ambapo ilianza kama homa ya kawaida lakini baadaye akawa anakosa pumzi hadi kupelekea kuwekewa mashine na kuchomwa sindano za kila siku zinazogharimu shilingi laki 7 kwa siku