Zaidi ya watu 800 wamefariki dunia baada ya tetemeko la ardhi nchini Morocco
Zaidi ya watu 800 wamefariki dunia baada ya tetemeko la ardhi nchini Morocco:
Zaidi ya watu 800 wamefariki dunia baada ya tetemeko la ardhi kutokea nchini Morocco Ijumaa usiku.
Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo imesema watu wengine zaidi ya 600 wamejeruhiwa katika janga hilo.
Tetemeko hilo kubwa lisilo la kawaida limesababisha uharibifu wa majengo katika vijiji vya milima ya Atlas hadi kwenye mji wa kihistoria, #Marrakech.
Wengi wa waliokufa ni kutoka katika mikoa mitano iliyo karibu na eneo lililoathiriwa zaidi na tetemeko hilo.
Idadi ya vifo na majeruhi inatarajiwa kuongezeka wakati waokoaji wakifukua vifusi vya majengo yaliyoanguka na wakijaribu kuyafikia maeneo yasiyofikika kwa urahisi.