Tunapitia Maumivu yasiyovumilika-Familia ya Lokassa ya Mbongo
Tunapitia Maumivu yasiyovumilika-Familia ya Lokassa ya Mbongo
“Ni fedheha”, miezi saba baada ya kifo chake bado hajazikwa.
Familia ya mpiga gitaa maarufu wa Congo Lokassa ya Mbongo inasema inapitia “maumivu yasiyovumilika” na “fedheha” wakati wakisubiri usaidizi wa serikali ili kumzika mpiga gitaa huyo ikiwa ni karibu miezi saba baada ya kifo chake.
Mwanawe André Marie Lokassa aliambia BBC kwamba serikali iliahidi kusaidia kuandaa mazishi ambayo “atastahili” kutokana na jina la nyota huyo wa muziki, lakini hadi sasa imeshindwa kufanya hivyo.
Bw Lokassa aliambia BBC kwamba familia hiyo iliwasilisha ombi la bajeti ya $75,000 (£61,000) kwa ajili ya mazishi, lakini bado halijaidhinishwa, na kuacha familia katika sintofahamu.