Shamba ekari 100 Mkuranga kwa ajili ya kupanda miti dawa
“Waziri Mkuu wa India amekubali ombi la Tanzania kuanzisha kituo cha tiba asilia ambapo tumenunua shamba ekari 100 Mkuranga kwa ajili ya kupanda miti dawa ambayo tunaijua ili kuweza kutengeneza dawa.
Hata hivyo tiba asili tayari imeanzishwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa saba na tunawaomba madaktari waweze kushauriana na wagonjwa ili kujadili tiba gani iweze kutumika katika matibabu.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema katika Miaka miwili ya SSH Rais Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi Trilioni 6.7 kwa ajili ya Sekta ya Afya.
Waziri Ummy amesema hayo wakati akijibu Maswali ya Waandishi wa Habari katika Mkutano ulioandaliwa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ili kuelezea mafaniko ya ziara ya Rais Samia nchini India.