Waziri Mkuu Atembelea shamba la Kisasa la Mifugo -Italia
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea shamba la ufugaji wa ng’ombe wa maziwa la Alesandra lililopo Milan nchini Italia, ambalo linaendeshwa kwa kutumia mifumo ya kisasa ya kielektoniki ikiwemo ukamuaji wa maziwa kwa kutumia roboti.
Akiwa katika shamba hilo lenye takribani ng’ombe 500 Waziri Mkuu Majaliwa ameshuhudia mifumo bora ya ufugaji, ulishaji, unyonyeshaji na ukamuaji wa maziwa, ambapo ng’ombe mmoja ana uwezo wa kutoa lita kuanzia 35 hadi 70 kwa siku.
Waziri Mkuu ameeleza kufurahishwa na teknolojia inayotumika katika ufugaji huo.
Waziri Mkuu Majaliwa yupo nchini Italia akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la Chakula Duniani.