News
Ukungu mkubwa wasababisha ajali ya magari 158 huko New Orleans Marekani
Ukungu mkubwa wasababisha ajali ya magari 158 huko New Orleans Marekani.
Watu 25 walijeruhiwa katika ajali iliyotokea eneo la Interstate 55 katika Parokia ya St John the Baptist, walisema polisi, ambao walionya kwamba idadi ya vifo inaweza kuongezeka.
Ukungu mzito na moshi kutoka kwa moto ulichanganyika na kupunguza mwonekano wa magari yanayosafiri siku ya Jumatatu, hali ambayo ilipelekea ajali hiyo.
Tazama kwenye hii Picha kutoka eneo la tukio, ikionyesha msururu wa magari 158 yaliyohusika katika ajali hiyo.