Kiharusi na mshtuko wa moyo husababisha asilimia 73% ya vifo barani Afrika
Kwa Mujibu wa takwimu za Shirika la afya Duniani(WHO);
Ugonjwa wa Kiharusi(stroke) pamoja na mshtuko wa moyo au shambulio la moyo(heart attacks) husababisha asilimia 73% ya vifo vyote vya moyo na mishipa ya damu katika ukanda wa Afrika,
Ili kuzuia Ugonjwa wa kiharusi, ni muhimu kuelewa sababu hatarishi za kupata kiharusi.
Hapa kuna baadhi ya hatua za kupunguza hatari ya kupata Ugonjwa wa kiharusi;
– Epuka au Acha kabsa Uvutaji wa Sigara
– Epuka matumizi ya Pombe kupita kiasi
– Dhibiti shinikizo lako la Damu kuwa katika kiwango kinachotakiwa,
hivo kama una Shinikizo la juu la damu(high blood pressure) hakikisha unalidhibiti.
– Dhibiti kiwango cha juu cha Lehemu au Cholestrol mwilini
– Hakikisha unakula mlo bora na wenye afya( A healthy diet)
– Dhibiti ugonjwa wa Kisukari
– Dhibiti Uzito wako wa mwili na kuepuka tatizo la kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi(Overweight).
#PICHA: WHO Steps to reduce Risk of Stroke;