Mji wa Gaza sasa umezingirwa kabisa, Msemaji wa Jeshi atoa Taarifa
Wakati imepita usiku wa manane huko London, 02:00 asubuhi huko Gaza na Israeli, na 03:00 nchini Uturuki – ambapo mwanadiplomasia mkuu wa Marekani amewasili kwa mazungumzo Mashariki ya Kati.
Hii inafuatia ziara ya Antony Blinken katika Ukingo wa Magharibi na Iraq siku ya Jumapili wakati wa msafara wa kidiplomasia katika eneo hilo. Amekuwa akijadili juhudi za kuzuia mzozo wa Gaza kuenea na anaendelea kushinikiza kusitishwa kwa mapigano.
Mwandishi wa BBC Anthony Zurcher anadokeza kuwa anajaribu kutafuta suluhisho kwa pande zote. Waziri Mkuu wa Israel amekataa wazo la kusitishwa kwa misaada ya kibinadamu kwa sasa, huku majirani wa kiarabu wa Israel wakitoa wito wa kusitishwa kwa mapigano mara moja.
Uhusiano wa Uturuki na Israel umezidi kudorora huku idadi ya vifo katika mzozo huo ikiongezeka.
Wakati huo huo, Israel inasema vikosi vyake vimeigawanya Gaza mara mbili baada ya mashambulizi yake ya ardhini dhidi ya Hamas kufika katika pwani ya Mediterania katika ardhi ya Palestina.
Msemaji wa jeshi alisema kuwa mji wa Gaza sasa umezingirwa kabisa.
Kumekuwa na mashambulizi ya angani na milipuko mikubwa kaskazini mwa eneo hilo – ambayo ni mikali zaidi tangu vita kuanza, mwandishi wa BBC katika Ukanda wa Gaza amesema. Huduma za simu na intaneti zimekatwa tena.
Umoja wa Mataifa – ambao ni makazi ya watu wengi wa Gazan milioni 1.5 waliotoroka makazi yao – unasema maeneo 48 ya Ukanda wa Gaza yameharibiwa tangu vita vilipoanza.
Source: Bbc