Afisa Polisi Akamatwa kwa Kupokea Rushwa ili kuwaachia Mahabusu nchini Kenya
Afisa mmoja wa Polisi Amekamatwa baada ya kupokea Rushwa nchini kenya, Afisa huyo alipewa kiasi cha KSh 3k ili Kuwaachilia Huru Mahabusu.
Taarifa zinasema Afisa huyo wa polisi alikamatwa kwa madai ya kuchukua hongo ili kuwaachilia washukiwa wanne waliokuwa walevi na wafanya fujo licha ya kuwa kizuizini,
Afisa Mkuu wa Kituo (OCS) Duncan Otieng alishtakiwa kwa kuweka KSh 3000 mfukoni na alinaswa na kupelekwa Integrity Centre.
Washukiwa waliokamatwa Ijumaa, Novemba 3, waliwekwa rumande na kusubiri kufikishwa mahakamani Jumatatu, Oktoba 6,
Ripoti ya polisi ambayo TUKO.co.ke iliisoma ilisema kuwa alikamatwa na maafisa wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC).