Simba Yamtimua kocha baada ya kichapo cha Yanga
Klabu ya Simba imevunja mkataba na kocha wake mkuu Roberto Oliveira siku mbili baada ya kukubali kichapo kizito cha goli 5-1 kutoka kwa wapinzani wao wa Yanga
Kocha huyo raia wa Brazil maarufu kwa jina la Robertinho alijiunga na Simba akitokea klabu ya Vipers ya Uganda mwezi Januari mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula, makubaliano ya kuvunja mkataba yanefikiwa na pande zote mbili, klabu na kocha mwenyewe.
Simba pia imesitisha mkataba na kocha wake wa viungo Corneille Hategekimana.
Unazungumziaje uamuzi huu wa Klabu ya Simba?