Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Achoma nyumba moto,kisha kujaribu kujiua kwa kujichoma kisu shingoni kwa sababu ya wivu wa mapenzi

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza linamshikilia Joseph Hezron (54), mkazi wa Bukara wilayani Sengerema kwa kuchoma moto nyumba ya mpenzi wake aitwaye Lucy James, kisha kujaribu kujiua kwa kujichoma kisu shingoni huku chanzo kikitajwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Tukio hilo limetokea Novemba 9, 2023 katika mtaa wa Bukara baada ya Joseph kumtuhumu mpenzi wake huyo kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine aitwaye Jelemia Kamambi, ndipo alichoma nyumba hiyo na kupelekea hasara.

Uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kuwa mwanaume ambaye Joseph alikuwa anamtuhumu hakuwa mpenzi wa mwanamke huyo (Lucy Hezron) bali alikuwa kaka yake, hivyo kuwataka wanaume kuacha wivu wa mapenzi uliopitiliza.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.