Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Babu Tale hatarini kufungwa jela kutokana na kushindwa kumlipa Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde

Hatima ya Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Hamisi Shabani Taletale, maarufu kama Babu Tale, sasa itajulikana Ijumaa, Novemba 17, mwaka huu wakati Mahakama Kuu Kanda ya Dare es Salaam itakapotoa uamuzi wa shauri la maombi ya kumpeleka jela kutumikia kifungo.

Babu Tale ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni inayojihusisha na shughuli za burudani, Tip Top Connections Company Limited yuko hatarini kufungwa jela kutokana na kushindwa kumlipa Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde, fidia ya Sh250 milioni.

Sheikh Mbonde amefungua maombi Mahakama Kuu dhidi ya Tip Top na Babu Tale akiiomba Mahakama hiyo iamuru Babu Tale akamatwe na afungwe kwa kushindwa kumlipa fidia hiyo.

Wakili wa Sheikh Mbonde, Loveness Ngowi amelieleza Mwananchi leo Jumatatu, Novemba 13, 2023 kuwa maombi hayo yamesikilizwa na Jaji Wilbert Chuma Novemba 6 na kwamba sasa amepanga kutoa uamuzi Ijumaa Novemba 17, 2023.

Hata hivyo, wakili wa Babu Tale aliyekuwepo siku ya usikilizwaji wa maombi hayo ya Sheikh Mbonde hakuwa tayari kusema lolote akidai kuwa hana hakika na hakumbuki kama uamuzi wa shauri hilo umepangwa lini.

Mwaka 2013, Sheikh Mbonde alifungua kesi ya madai dhidi ya kampuni hiyo ya Tip Top, akidai imlipe fidia ya Sh750 milioni kwa kosa la ukiukwaji wa haki miliki, kwa kutumia kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake kinyume cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki

Source: Tanzaniaweb

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass