Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

FAHAMU KUHUSIANA NA TATIZO LA MATEGE(RICKETS)

MATEGE

• • • • • •

FAHAMU KUHUSIANA NA TATIZO LA MATEGE(RICKETS)

Kwa kawaida mifupa inatengenezwa na  Mchanganyiko wa protini (osteoid) na madini kama calcium na phosphate. Kutokuwapo kwa madini haya kunapelekea mifupa kuwa laini na rahisi kuvunjika kwa watoto na hata watu wazima. 

Matege ni tatizo linayoikumba mifupa inayokua na inasababishwa na kutokuwapo kwa madini hasa katika sehemu za mifupa zinazohusika na ukuaji kabla ukuaji haujafikia ukomo. Kutokuwepo kwa madini husababisha mifupa hii kuwa laini sana na hivyo kupinda kwa urahisi hasa kutokata na uzito wa mwili au nguvu ya mvutano itokanayo na misuli. 

SABABU

1. kimsingi matege husababishwa na ukosefu wa vitamini D

2. Ukosefu wa madini aina ya calcium na phosphate

3. Matatizo katika figo

Kula vyakula vyenye upungufu wa vitamin D na madini husika, kutumia dawa zinazokinzana na calcium, kutumia dawa zenye aluminium kwa ajili ya kuzuia asidi na magonjwa ya figo yanayoongeza kiwango cha kutolewa kwa madini haya mwilini vyote vinapelekea tatizo hili.

DALILI

1. Kudumaa

2. Kujihisi huna nguvu na kutokuwa na hamu ya kufanya chochote

3. Tumbo kuongezeka ukubwa

4. Misuli kulegea na kukosa nguvu

5. Kuvunjika kwa mifupa

6. Dege dege 

7. Kukakamaa

8. Kutoa kisauti wakati wa kupumua.

Katika kichwa dalili zake ni

1. Kulainika kwa mifupa ya kichwa 

2. Komo la mbele kuongezeka

3. Kuchelewa kuota meno

4. Kuchelewa kufunga kwa uwazi wa kichwa

Kifuani

1. Maambukizi katika mfumo wa upumuaji

2. Kuvimba kwa kiunganishi kati ya sehemu ya mbavu na cartilage na hivyo kupangana kama chembe ya rozari

3. Kutokea kwa kishimo mwisho wa mbavu wakati wa kupumua

Mgongoni

1. Kupinda kwa sehemu mbalimbali za mgongo

Miguuni

1. Kuongezeka kwa upana wa vifundo vya miguu na mikono

2. Maumivu ya miguu

3. Matatizo katika nyonga 

4. Kupinda kwa miguu

DAKTARI WAKO ATATAKA KUJUA YAFUATAYO

1. Aina ya vyakula unavyompa mwanao

2. Muda ambao mwanao anautumia akiwa nje (juani), aina ya mavazi anayovaa kwani jua linahusika katika utengenezaji wa vitamin D

3. Dawa anazotumia mtoto kwamfano matumizi ya dawa za degedege kunaongeza kuvunjwavunjwa kwa vitamin D na matumizi ya baadhi ya dawa zenye aluminium hupunguza kufyonzwa kwa phosphate 

4. Matatizo ya figo.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.