Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO KWA MAMA MJAMZITO

 MSONGO WA MAWAZO

• • • • •

MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO KWA MAMA MJAMZITO


Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuchangia hali ya Msongo wa Mawazo kwa mama Mjamzito, na baadhi ya sababu hizo ni kama vile;


– Mama mjamzito kupigwa au kujeruhiwa katika ajali mbali mbali


– Ujauzito wake kukataliwa na mtu aliyempa huo ujauzito


– Au changamoto mbali mbali katika maisha yake ya mahusiano


– Mama mjamzito kufukuzwa kazi


– Mama mjamzito kutengana na mume wake


– Mama mjamzito kufiwa na mtu wake wa karibu kama baba,mama,mume N.K


– Pia changamoto mbali mbali za kiuchumi kama vile kukosa pesa kabsa za matunzo, Kukosa pesa kwa ajili ya chakula N.K


MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO KWA MAMA MJAMZITO


Tafiti mbali mbali za wataalam wa afya zinasema kwamba,Msongo wa Mawazo ambao mama mjamzito huwa nao, huweza kusababisha athari mbali mbali zikiwemo zile zinazotokea wakati wa uumbaji wa mtoto, na wakati mwingine hata watoto kuzaliwa na ulemavu flani katika mwili.


Athari za mama mjamzito kuwa na msongo wa mawazo au kwa kitaalam tunaita Severe depression, huweza kutokea kabla,wakati na baada ya mtoto kuzaliwa.


• Ujauzito huweza kutoka wenyewe kama mama mjamzito akiwa na hali ya msongo wa mawazo kupita kiasi.


• Mama huweza kujifungua mtoto mwenye ulemavu flani kama vile tatizo la Midomo Sungura ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Cleft lip and cleft palate au kuzaa mtoto mwenye shida ya Mgongo wazi ambapo kwa kitaalam hujulikana kama spinal bifida.


• Kama Msongo wa mawazo utaendelea hata baada ya mama kujifungua, huweza kupelekea madhara makubwa zaidi hata kufikia hatua ya kutoa uhai wa mtoto aliyezaliwa au mama kujiua mwenyewe.


DALILI ZA MAMA MJAMZITO MWENYE MSONGO WA MAWAZO NI PAMOJA NA;


– Mama mjamzito kufanya kazi moja kwa masaa mengi,Mfano; Mama mjamzito huweza kufagia eneo dogo tu lakini kwa masaa mengi anafanya kazi hyo hyo moja tu


– Mama mjamzito kuanza kuongea mwenyewe mara kwa mara,hyo ni dalili pia ya msongo wa mawazo


– Mama mjamzito kuanza kuongelea mambo yanayohusu kujiua mwenyewe au kuua mtoto aliyetumboni au atakayezaliwa


– Mama mjamzito kuanza kuomba msamaha kila mara kwa watu,hata kama kitu alichokifanya sio kosa kabsa katika hali ya kawaida


– Mama mjamzito kukosa usingizi kabsa na wakati mwingine akilala anaweweseka sana usku


KUMBUKA; Ukiona mtu unayekaa naye ana dalili kama hizi msaidie mapema kwa kumpeleka kwa wataalam wa afya ili kuepusha madhara makubwa ambayo huwe za kutokea hapo baadae.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.