Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

MAMBO YAKUFANYA ILI KUJIKINGA NA UGONJWA WA FANGASI

 FANGASI

• • • • •

MAMBO YAKUFANYA ILI KUJIKINGA NA UGONJWA WA FANGASI

Watu wengi hawajui kwamba Fangasi huweza kushambulia maeneo mengi sana katika mwili wa binadamu, Wengi wao hujua fangasi wa Miguuni tu. Fangasi huweza kushambulia maeneo mbali mbali katika mwili wa Binadamu kama Ifuatavyo;

✓ Kuna Fangasi wa kwenye Damu

✓ Kuna Fangasi wa miguuni pamoja na vidole vyake

✓ Kuna fangasi wa kwenye Viganja vya mikono pamoja na vidole vyake

✓ Kuna Fangasi wa Sehemu za siri za mwanamke na mwanaume

✓ Kuna Fangasi wa mdomoni

✓ Kuna Fangasi wa kwenye Ulimi

✓ kuna Fangasi wa kwenye koo

N.K

• Soma: Chanzo cha Tatizo la Kwikwi na Tiba yake

MAMBO YAKUFANYA ILI KUJIKINGA NA UGONJWA WA FANGASI NI PAMOJA NA;

• Epuka kuvaa Viatu vibichi au vyenye majimaji au Soksi Mbichi,hii itakusaidia kujikinga na Fangasi wa Miguuni.

• Epuka kuvaa Nguo za ndani Mbichi au zenye unyevu unyevu hii itakusaidia kujikinga na Fangasi wa Sehemu za Siri.

• Zingatia usafi wa mwili hasa hasa sehemu za siri, hii itakusaidia sana usipate Fangasi mara kwa mara Mfano; Kwa mama mjamzito ambaye kinga ya mwili imeshuka kwa sababu ya Ujauzito huwa katika hatari ya kushambuliwa na magonjwa kwa Urahisi kama vile FANGASI wa Ukeni na UTI.

• Epuka kushiriki mapenzi Kwa Njia Ya Mdomo na mtu mwenye tatizo hili la Fangasi, au epuka kubusiana(kissing) hasa hasa na yule ambaye anasumbuliwa na Fangasi wa ulimi na Mdomoni.

• Epuka matumizi ya dawa hovio,kwani dawa zingine huweza kushusha kinga ya mwili na kukupelekea kushambuliwa na Magonjwa kama Fangasi kwa urahisi.

• Epuka matumizi ya dawa au sabuni zenye kemikali ambazo huweza kubadilisha hali ya ndani ya uke,ikiwemo hali ya acid,kuleta ukavu,na kusababisha mwanamke kupata fangasi wa ukeni kwa urahisi.

KUMBUKA; Fangasi huweza kuonyesha dalili tofauti tofauti kulingana na eneo la mashambulizi ya Fangasi hao. 

• Soma: Chanzo cha Tatizo la Kwikwi na Tiba yake

DALILI HIZO ZA TATIZO LA FANGASI NI PAMOJA NA;

– Kupatwa na miwasho sana sehemu za Siri pamoja na maeneo mengine ambapo fangasi wameshambulia kama vile Miguuni na kwenye Vidole

– Ngozi ya sehemu za siri kuzunguka mashavu ya uke,pamoja na ngozi ya korodani kubadilika rangi na kuwa Nyekundu

– Kupata michubuko maeneo ya sehemu za siri na sehemu zingine ambazo fangasi wameshambulia kama kwenye mikono na miguuni

– Kutokwa na uchafu kama maziwa mgando ukeni

– Sauti kubadilika na kuanza kukwaruza hasa hasa kwa mgonjwa mwenye Fangasi wa kooni

– Mgonjwa wa fangasi kooni hupata shida ya kula au kumeza kitu chochote

MATIBABU YA UGONJWA WA FANGASI

Matibabu ya Fangasi hutegemea sana na eneo ambalo fangasi wameshambulia,hivo matibabu ya Fangasi huhusisha dawa mbali mbali kama vile; Clotrimazole Cream,au Clotrimazole ya tubu za kuweka ukeni.

• Soma: Chanzo cha Tatizo la Kwikwi na Tiba yake

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.