Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

JINSI YA KUBORESHA MFUMO WA MMENG’ENYO WA CHAKULA MWILINI

 CHAKULA

• • • • • •

JINSI YA KUBORESHA MFUMO WA MMENG’ENYO WA CHAKULA MWILINI


Baadhi ya mambo muhimu ya kufanya na kuzingatia ili kuboresha na kuimarisha mfumo wa mmeng’enyo wa chakula kwenye mwili wako,


✓ Kula zaidi matunda ambayo yana asili ya nyuzi nyuzi au Fibers kama vile; machungwa,maembe n.k


✓ Pia ulaji wa Tende, mapapai,maparachichi husaidia sana katika kurahisisha umeng’enyaji wa chakula mwilini


✓ Tafuna vizuri chakula chako, huku ukiepuka tabia ya kula chakula huku unaongea hali ambayo huweza kupelekea gesi au hewa kujaa tumboni


✓ Jenga utaratibu wa kunywa maji ya kutosha kwa siku angalau lita 2.5 mpaka 3


✓ Kula vyakula ambavyo vina kiwango kikubwa cha mafuta salama mfano; omega-3 fatty acids kama vile Samaki wakubwa,dagaa n.k


✓ Epuka msongo wa mawazo,watu wengi hawajui kwamba msongo wa mawazo huweza kuleta athari hadi kwenye mfumo mzima wa umeng’enyaji chakula mwilini


✓ Kufanya mazoezi ya mwili kila siku huboresha sana mfumo wako wa umeng’enyaji chakula mwilini


VITU AMBAVYO HUATHIRI UMENG’ENYAJI WA CHAKULA MWILINI


– Unywaji wa pombe kupita kiasi


– Uvutaji wa sigara


– Tabia ya kuchelewa sana kula chakula usiku, 


pamoja na kula chakula kingi usiku halafu unaenda kulala

N.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.


Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.