Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Tatizo la Kukojoa Mara kwa Mara,chanzo chake na Tiba

Tatizo la Kukojoa Mara kwa Mara,chanzo chake na Tiba

Kukojoa mara kwa mara baada ya kupata kinywaji, Unaweza kupatwa na hali ya kukojoa mara kwa mara baada ya kunywa vinywaji vingi kama vile Maji mengi, vinywaji vyenye Caffeine,Pombe n.k

Hali ambayo wakati mwingine inaweza kuleta usumbufu hasa wakati ukiwa Umelala Usiku,

Lakini pia Kukojoa Mara kwa Mara inaweza kuwa kiashiria cha kukuonyesha kwamba kuna kitu hakipo Sawa,

Haya hapa ni baadhi ya Matatizo ambayo kiashiria chake Mojawapo ni Mtu kukojoa Mara Kwa Mara;

1. Mtu kuwa na matatizo kwenye Kibofu cha Mkojo

2. Mtu kuwa na matatizo kwenye Figo,Ureter n.k

3. Mtu kuwa na tatizo la KISUKARI

4. Mtu kuwa na matatizo kwenye tezi dume yaani prostate gland problems

5. Mtu kuwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo yaani urinary tract infection-UTI

6. Mtu kuwa na tatizo la kuvimba kwa Urethra yaani urethritis

7. Mtu kuwa na Uvimbe kwenye eneo la Pelvic, Uvimbe kwenye kibofu cha Mkojo n.k

8. Hali ya Kuwa Mjamzito, wakina mama wengi wajawazito hupatwa na hali ya kukojoa mara kwa mara,

Hii ni kutokana na Presha au mgandamizo wa mtoto anayekuwa tumboni dhidi ya kibofu cha Mkojo, hali ambayo hupelekea eneo(room) kwenye kibofu cha Mkojo kupungua,

9. Mtu Kupatwa na tatizo la kuvimba kwa kuta za kibofu yaani kwa kitaalam hujulikana kama interstitial cystitis

10. Mtu kupatwa na tatizo la Mawe kwenye Njia ya Mkojo(urinary tract stones)

11. Matumizi ya baadhi ya dawa kama vile dawa jamii ya diuretics

12. Huduma ya radiotherapy

13. Kushambuliwa na magonjwa mbali mbali ya Zinaa(sexually transmitted infections (STIs)

14. Mtu kuwa na matatizo ya Neva yaani neurological problems n.k

MATIBABU YAKE NI YAPI?

Matibabu ya tatizo hili hutegemea na chanzo chake,kama nilivyokwisha kueleza hapo Juu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.