Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Antibiotics hutibu maambukizi yanayosababishwa na Bacteria Pekee na Wala haziwezi kutibu Viruses

Antibiotics hutibu maambukizi yanayosababishwa na Bacteria Pekee na Wala haziwezi kutibu Viruses

Tumia Dawa Jamii ya Antibiotics kwa Usahihi wake, Dawa hizi hutibu tu baadhi ya maambukizi ambayo husababishwa na Bacteria kama vile;

– UTI,Strep throat,Whooping Cough n.k

Ila antibiotics haziwezi kufanya kazi kutibu maambukizi ambayo husababishwa na Viruses kama vile;

– Flu,Covid-19,Masundo sundo(genital warts) n.k

Matumizi ya Antibiotics sehemu ambapo hazihitajiki badala ya kukuletea faida huweza kukusababishia madhara,

Mwili wako unaweza kuonyesha matokeo mbali mbali kama umetumia dawa hizi isivyosahihi, kama vile;

• Kuanza Kupata vipele au rashes kwenye ngozi yako

• Mwili wako kuanza kuwasha sana

• Mtu kuhisi kichefuchefu na kutapika

• Mtu kupata kizunguzungu kikali

• Mtu kuharisha

• Mtu kupata maumivu ya tumbo n.k

USHAURI:

1. Sio kila Ugonjwa hutibiwa kwa Dawa Jamii ya antibiotics,hivo ongea na wataalam wa afya kwanza,upewe ushauri juu ya dawa sahihi kwako

2. Epuka kuzidisha kiwango cha Dawa Ulizoandikiwa eti ili upone kwa Haraka zaidi

3. Ukiona unapata reactions zozote baada ya kutumia dawa,unaweza kuuliza kujua ni sahihi au kuna kitu hakipo sawa.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.