Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Mtoto juu ya Mtoto,Mimba mara tu baada kutoka Kujifungua-Zingatia haya

Mtoto juu ya Mtoto,Mimba mara tu baada kutoka Kujifungua-Zingatia haya

Wanawake wengi baada ya kujifungua husubiri kwanza waone hedhi ndipo waanze kuchukua tahadhari ya kujikinga na Mimba,

Kumbuka hedhi ni matokeo ya kutokuwa na urutubishaji wa Yai, endapo yai limerutubishwa huwezi ona hedhi kama ulivyokuwa unasubiria ndipo uanze kujikinga,

Hii imepelekea wanawake wengi kubeba mimba ambazo hazijapangwa baada ya kujifungua,

Una mimba nyingine na huku bado unanyonyesha,

Kumbuka Pia kwa baadhi ya wanawake huchelewa Sana kupata hedhi yao ya kwanza toka Kujifungua,

Kumekuwa na Ongezeko kubwa la Wanawake ambao wanajikuta Tayari Wana Mimba wakati watoto wao bado ni wachanga kabsa,

Hii huwafanya kuwa na Msongo zaidi wa mawazo hata kupelekea kushindwa kumhudumia vizuri mtoto ambaye tayari kazaliwa.

Wengi wao ukiawauliza,watakuambia Mimi nilikuwa nasubri kupata HEDHI YANGU ndipo niaze kuchukua tahadhari,

Sasa Leo nimekupa elimu hii japo kidogo, Ufahamu kwamba hedhi ikija ujue ni matokeo kwamba yai halijafanikiwa kurutubishwa,

lakini kama mzunguko wako wa hedhi umekaa Sawa,yai likatoka kwenye Vifuko vya mayai(Ovaries), Kisha ukafanya mapenzi bila tahadhari yoyote,unaweza kabsa kupata Ujauzito na Swala la kuona hedhi isilione kabsa,

JIKINGE NA MIMBA AMBAZO ZIPO NJE YA MPANGO

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.