Naombeni Msaada,Rotarix ni Chanjo ya Nini? maana Nmeona kwenye kadi la Mwanangu
Naombeni Msaada,Rotarix ni Chanjo ya Nini? maana Nmeona kwenye kadi la Mwanangu
Rotarix Chanjo ya kuzuia Magonjwa ya kuhara yanayosababishwa na Rotavirus
Chanjo ya kuzuia magonjwa ya kuhara yanayosababishwa na RotaVirus Hujulikana kwa jina la Rotarix,
Rotarix ndyo chanjo ambayo mtoto mchanga hupewa ili kumkinga na Ugonjwa huu wa Kuharisha ambao chanzo chake ni RotaVirus
Magonjwa ya kuhara husababishwa na vimelea vya aina mbalimbali.
Vimelea vya Rotavirus huchangia kwa kiwango kikubwa katika magonjwa ya kuhara kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.
Nchini Tanzania takwimu za mwaka 2008 zinaonyesha kuwa magonjwa ya kuhara yasababishwayo na rotavirus yalichangia asilimia 30 – 50 kwa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano waliolazwa kwa ugonjwa wa kuharisha.
Ugonjwa wa kuhara unaosababishwa na vimelea vya Rotavirus huenezwa kwa njia ya kula au/na kunywa maji yaliyochafuliwa na kinyesi chenye virusi hivyo.
Dalili zake ni pamoja na;
– Mtoto Kuharisha
– Mtoto kuwa na homa
– Mtoto Kutapika,
– Kuwa na Dalili za kupungukiwa maji na chumvichumvi mwilini
– Mtoto akiharisha sana hulegea ikifuatiwa na Degedege na kupoteza fahamu
– Upungufu mkubwa wa maji na chumvichumvi mwilini husababisha kifo.
– Aidha, husababisha utapiamlo, kudumaa na mtindio wa ubongo.
Ugonjwa huu hukingwa kwa chanjo mbili za Rotavirus zinazotolewa wiki ya 6 na wiki ya 10.
Namna nyingine ya kuwakinga watoto dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu ni Kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa miezi sita pamoja na Kuimarisha usafi wa mazingira na kunawa mikono kwa maji safi na sabuni.
Cr: Mpango wa Taifa wa Chanjo Tanzania