Watoto 14,000 nchini Kenya huzaliwa kila mwaka na ugonjwa wa Sickle Cell
Watoto 14,000 nchini Kenya huzaliwa kila mwaka na ugonjwa wa Sickle Cell
Kiwango cha chini au kuanzia Watoto 14,000 nchini Kenya huzaliwa kila mwaka na ugonjwa wa Sickle Cell
Kutokana na kukosekana kwa uchunguzi wa watoto wachanga na matibabu yanayofaa, wengi wa watoto hawa hufa bila kutambuliwa utotoni kutokana na sababu zinazoweza kuzuilika kama vile malaria na maambukizi ya bakteria.
Ugonjwa huu hutokea sana kote nchini Kenya huku kaunti 17 zikiwa na mzigo mkubwa zaidi katika maeneo ya Magharibi na Pwani na Nairobi.
๐ช๐ต๐ฎ๐ ๐ถ๐ ๐ฆ๐ถ๐ฐ๐ธ๐น๐ฒ ๐๐ฒ๐น๐น ๐๐ถ๐๐ฒ๐ฎ๐๐ฒ?
Sickle Cell Disease is an inherited blood disorder where the red blood cells become hard and sticky and looks like a C-shaped farm tool called a โSickleโ. SCD is inherited from both parents; sickle cell trait is inherited fromโฆ pic.twitter.com/M6xreYffDf— Ministry of Health (@MOH_Kenya) June 19, 2023
Ugonjwa wa Sickle Cell ni ugonjwa wa kurithi wa damu ambapo chembe nyekundu za damu huwa ngumu na kunata na huonekana kama umbo la C “Sickle”.
Mtu mwenye Sickle Cell anaweza kuishi maisha marefu na kufanya shughuli zake ili mradi tu apatiwe uchunguzi wa mara kwa mara na daktari, anywe dawa mara kwa mara, azuie maambukizi kwa njia za usafi kama vile kunawa mikono na kunywa maji mengi.
Soma Zaidi hapa; Ugonjwa huu wa sickle cell au Seli Mundu