TANZIA:Mwanazuoni maarufu Sheikh Maalim Basaleh amefariki dunia
Sheikh Basaleh afariki dunia
Muktasari:
- Mwanazuoni maarufu Sheikh Maalim Basaleh amefariki dunia leo jioni akipatiwa matibabu katika hospitali ya Aga Khan alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki mbili, anatarajiwa kuzikwa kesho saa saba mchana.
Dar es Salaam. Mwanazuoni na sheikh maarufu Maalim Basaleh amefariki dunia leo Jumapili katika Hospitali ya Aga Khan alipokuwa akipatiwa matibabu akisumbuliwa na matatizo ya figo na saratani.
Mtoto wa marehemu Abdullatif Ali Basaleh amesema baba yake amefariki saa 12 jioni baada ya kulazwa kwa takribani wiki mbili na nusu akipatiwa matibabu hayo.Amesema mazishi ya baba yake yatafanyika kesho saa 7 mchana katika makaburi ya Kisutu.
“Leo baba amefariki dunia si muda mrefu kesho tutakwenda kumpumzisha baada ya swala ya Adhuhuri,” amesema Abdullatif.
Credits Source: To Mwananchi