Kazi yangu inahusu kuosha na kusugua meno maiti:Filinda Kamau raia wa Kenya
Filinda Kamau raia wa Kenya amejikuta akipata maarufu mtandaoni kwa kuchapisha video za TikTok zinazoonesha kazi zake katika chumba kimoja cha kuhifadhia maiti huko Nakuru.
Filinda hufanya kazi kama mhudumu wa kuosha na kutayarisha maiti.
Anasema anataka kuwasaidia watu kukomesha hofu ya vyumba vya kuhifadhia maiti na kumaliza unyanyapaa kwa watu wanaofanya kazi katika maeneo hayo.
Je umewahi kufikiria inakuaje kufanya kazi ya kukutana na maiti kila siku? je changamoto zake? na jamii na ndugu wanamchukuliaje?
Source:Bbcswahili #waridiwabbc #kenya