Muuguzi Lucy Letby wa nchini Uingereza amepatikana na hatia ya kuwaua watoto saba
Muuguzi Lucy Letby wa nchini Uingereza amepatikana na hatia ya kuwaua watoto saba, na kumfanya kuwa muuaji mkubwa zaidi wa watoto nchini Uingereza katika nyakati za hizi.
–
Aliwaua watoto hao kwa kuwadunga sindano ya hewa kati ya mwezi Juni 2015 na mwezi Juni 2016, alipokuwa akifanya kazi katika Hospitali ya Countess ya Chester.
–
Leby pia amepatikana na hatia ya kujaribu kuwaua watoto sita katika kitengo cha watoto wachanga cha hospitali hiyo, kwa njia ya kuwachoma sindano ya hewa kwa makusudi, kuwalisha kupita kiasi na kuwawekea sumu ya insulini.
–
Aligundulika baada ya uchunguzi wa miaka miwili wa Polisi kuhusu ongezeko la kutisha na lisiloelezeka la vifo vya watoto wachanga hospitalini hapo.
–
SOURCE: bbcswahili