Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Naibu Waziri Mkuu mpya Tanzania,Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu

Naibu Waziri Mkuu mpya Tanzania,Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemuhamisha aliyekuwa Waziri wa Nishati, Januari Makamba kutoka wizara hiyo na kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Taarifa iliyotolewa leo kutoka Ikulu imeeleza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje ni Stephen Byabato ambaye hapo awali alikuwa ni Naibu Waziri wa Nishati.

Aidha Rais Samia amemhamisha Balozi Pindi Chana kutoka kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu na Wizara ya Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

Katika taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Dk Moses Kasiluka imeeleza Rais Samia amemteua Anthony Mavunde kuwa Waziri wa Madini, awali alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo.

Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Jerry Silaa ameteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya Makazi.

Makame Mbarawa ameteuliwa kuwa Waziri wa Uchukuzi, awali alikuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.

Rais Samia pia amemuhamisha Waziri Innocent Bashungwa kutoka kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na kuwa Waziri wa Ujenzi.

Stergomena Tax amehamishwa kutoka kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Aidha, Mohammed Mchengerwa amehamishwa kutoka kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii na kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Tamisemi.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.