Shimo la ajabu linalowakosesha usingizi watafiti Duniani
Shimo hili lipo kwenye kona ya mbali ya Rasi ya Yamal kaskazini-magharibi mwa Siberia
Iilionekana ghafla na kwa mlipuko, na kuacha alama kubwa kwenye eneo hilo.
Lina kina cha futi 164 (m 50) linaweza kubeba sehemu muhimu za fumbo ambalo limekuwa likisumbuawanasayansi kwa miaka sita iliyopita tangu shimo la kwanza la ajabu kama hili lilipogunduliwa mahali pengine kwenye Rasi ya Yamal.
Bonde hili la hivi karibuni liligunduliwa na timu ya televisheni walipokuwa wakipita na wanasayansi wakati wa msafara na mamlaka za mitaa huko Yamal.
Shimo hili linafikisha jumla ya idadi ya mashimo yaliyothibitishwa huko Yamal na peninsula jirani ya Gydan kufikia 17.
Watafiti wengi kutoka Marekani na Urusi wanafika kuchunguza eneo hili.
Hadi sasa, watafiti wanasema kwamba milipuko hiyo inatokana na gesi, ambayo labda ni methane, inayojilimbikiza kwenye mifuko iliyotengwa kwenye eneo la tambarare.