Waziri Mkuu Thailand Awekwa Jela Miaka 8
Mahakama Kuu nchini Thailand imemhukumu Waziri Mkuu wa zamani wa Nchi hiyo Thaksin Shinawatra adhabu ya kifungo cha miaka nane jela.
Waziri Mkuu Shinawatra alikamtwa saa chache aliporejea nchini humo baada ya kuwa nje kwa muda wa miaka 15 ambapo adhabu aliyopewa inahusiana na hukumu zilizotolewa dhidi yake wakati alipokuwa nje ya Nchi.
Makosa yanayomkabili ni pamoja na matumizi mabaya ya mamlaka, kuiagiza benki inayoendeshwa na Serikali kutoa mkopo kwa Mteja wa nje kinyume cha sheria na pia kumiliki hisa kinyume cha sheria kwa kuwatumia Mawakala binafsi.