Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Bwana Harusi na Bibi Harusi waungua moto na kufariki

Watu takribani 100 wamefariki na wengine 150 wamejeruhiwa baada ya moto kuzuka kwenye sherehe ya ndoa katika Wilaya ya Hamdaniya, Jimbo la Nineveh nchini Iraq huku Wanandoa wote wawili (Bwana Harusi na Bibi Harusi nao wakiwa miongoni mwa waliofariki).

Naibu Mkuu wa Kurugenzi ya Afya ya Ninawi, Ahmed Dubardani amethibitisha kuwa Wanandoa hao wamefariki pia huku ikihofiwa kuwa idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka.

Idara za Ulinzi kwenye eneo hilo imesema moto huo uliwaka katika ukumbi wa harusi baada ya kurushwa fataki wakati shughuli hiyo ikiendelea.

Taarifa za awali zimesema jengo hilo limejengwa kwa vifaa vya ujenzi vinavyoshika moto kwa haraka, na kusababisha jengo kuanguka muda mfupi baada ya kushika moto.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.