News
Kuimarisha uhusiano baina ya Ufaransa na Uingereza
Paris: Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amefanya mazungumzo na Mfalme Charles wa III wa Uingereza hii leo mjini Paris, wakati kiongozi huyo alipoanza ziara ya siku tatu inayolenga kuangazia uhusiano baina ya Ufaransa na Uingereza.
Ziara hiyo ya Mfalme Charles iliyosubiriwa kwa muda mrefu inafanyika katikati ya maandamano dhidi ya mageuzi ya pensheni yanayotaka kufanywa na serikali ya Macron.