Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Mabadiliko ya tabia nchi huathiri Zaidi Vichanga – Ulaya

Wawakilishi kutoka Jumuiya ya Upumuaji ya Ulaya wametoa wito kwa Umoja wa Ulaya (EU) kupunguza viwango vya uchafuzi wa hewa, kwani vilivyopo vinahatarisha maisha ya watoto wachanga, wenye pumu na wenye magonjwa sugu ya mapafu.

Vichanga huathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi na uchafuzi wa hali ya hewa kwa kuwa mapafu yao yako kwenye hatua ya ukuaji na wao hupumua haraka na kuvuta hewa hadi mara tatu zaidi kuliko watu wazima wawapo nje.

Makundi mengine yaliyo hatarini ni pamoja na wagonjwa wa magonjwa sugu, wazee, Wajawazito na watu wanaofanya kazi za nje mfano za ujenzi.

Ripoti ya hivi karibuni ya Shirika la Afya Duniani (WHO) inaonesha kuwa hatua nyingi za kupunguza utoaji wa gesi chafuzi zinaweza kuwa chanzo cha hewa safi na kupunguza hatari za kiafya kwa makundi mbalimbali.

Forum Manager

Content creator&editor (Ms.Asifiwe)Jukumu langu kwako ni kuhakikisha unapata elimu ya kutosha pamoja na Updates mbali mbali ndani ya http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.