News
Wanasayansi wakuza kiinitete cha Binadamu bila mbegu za Kiume
Wanasayansi wakuza kiinitete cha Binadamu bila mbegu za Kiume:
Wanasayansi wamekuza kiinitete ambacho kinafanana kwa karibu na kiinitete cha mtoto wa siku 14 bila kutumia mbegu za kiume, mayai au tumbo la uzazi.
Timu ya Taasisi ya Weizmann ilisema “mfano wao wa kiinitete”, uliotengenezwa kwa kutumia seli shina, ulitoa homoni ambazo zilibadilisha kipimo cha ujauzito kuwa chanya kwenye maabara.
Matarajio ya mfano huo wa kiinitete ni kutoa njia ya kimaadili ya kuelewa nyakati za mwanzo za maisha yetu.
Source:bbc