HESLB waongeza Siku 7,dirisha la kuwasilisha maombi
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) @heslb_tanzania imetoa taarifa Wanafunzi waombaji mikopo ya elimu kwa ngazi ya Stashahada(Diploma) na umma kwa ujumla kuwa dirisha la kuwasilisha maombi kwa njia ya mtandao litakuwa wazi hadi Jumapili October 29, 2023.
Uamuzi wa kuongeza muda wa siku saba (7) unalenga kutoa fursa kwa waombaji wenye sifa ambao hawajaomba au hawajakamilisha maombi yao, kuomba na kukamilisha maombi yao ndani ya muda ulioongezwa.
Awali dirisha lilifunguliwa Jumamosi October 07,2023 na lilipanga kufungwa Jumapili October 22,2023.