Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Mauaji yakatisha mechi ya ubelgiji na Sweden

Mchezo wa kuwania kufuzu mashindano ya Euro 2024 kati ya Ubelgiji na Sweden usiku wa kuamkia leo ulikatishwa wakati wa mapumziko kwa sababu za kiusalama baada ya raia wawili wa Sweden kuuawa kwa risasi jijini Brussels.

Mauaji hayo yalitokea saa chache kabla ya mchezo huo tukio ambalo limechukuliwa kama ugaidi.

Wachezaji na mashabiki walitakiwa kusalia ndani ya uwanja kwa zaidi ya saa moja baada ya mchezo kukatishwa kwa ajili ya usalama wao.

Timu ya Sweden imesema ilipata taarifa za mauaji hayo wakati wa mapumziko na ikakubaliana kwamba ni vema wasiendelee na mchezo kwa heshima ya watu hao waliouawa.

Bado haijafahamika kama waathirika hao walikuwa jijini Brussels kwa ajili ya kuangalia mchezo huo.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.