Wanahistoria nchini Poland wamegundua mabaki ya mtoto wa karne ya 17
Wanahistoria nchini Poland wamegundua mabaki ya mtoto wa karne ya 17.
Wanahistoria nchini Poland wamegundua mabaki ya mtoto wa karne ya 17,aliyekutwa amefungwa kwa kutumia kufuli kwenye kaburi lake ili kumzuwia asifufuke kwenda kula binaadamu,
Wanahistoria hao wanaamini kwamba jambo hilo walilolikuta ni sehemu ya imani za kishetani.
Mifupa ya msichana huyo mdogo, ndio ya hivi karibuni kukutwa katika makaburi ya Kaskazini mwa kijiji cha Pien huko Poland.
Kwa kawaida makaburi hayo huzikwa watu waliotelekezwa, walioogopewa sana kwa kudhaniwa kuwa na mafungamano na nguvu za kishetani.
Je unaamini kweli mambo haya yana nafasi katika karne hii? Tupe mtazamo wako.