Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Andry Rajoelina achaguliwa tena kuwa rais wa Madagascar

Tume ya uchaguzi yasema Rajoelina mwenye umri wa miaka 49, amepata asilimia 58.95 ya kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi iliyofanyika Novemba 16.

Tume ya uchaguzi nchini Madagascar imetangaza hii leo kuwa rais aliyopo madarakani Andry Rajoelina ameshinda kwa mara nyingine katika duru ya kwanza ya uchaguzi ambao ulisusiwa na takriban wagombea wote wa upinzani.

Tume hiyo imesema Rajoelina mwenye umri wa miaka 49, amepata asilimia 58.95 ya kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi iliyofanyika Novemba 16.

Idadi ya waliojitokeza kupiga kura ilikuwa ndogo baada ya wagombea 10 kati ya 12 wa upinzani kutoa wito wa kususia uchaguzi huo wakilalamika kuwa ni “mapinduzi ya kitaasisi” kwa faida ya mgombea aliye madarakani

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.